Mji Mukufu wa Karbala jana ulitawaliwa na huzuni kubwa na hali ya maombolezo pindi Waumini walipokuwa wakisubiri kuwasili kwa mwili wa Ayatollah Imam Shahidi Sayyid Ali Khamenei (ra) kwa ajili ya shughuli za kutoa heshima zao za mwisho.
Kwa Mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) –ABNA– Hali ya huzuni ilitanda katika Mji Mtukufu wa Karbala pindi maelfu ya waumini wakisubiri kwa hamu kuwasili kwa mwili wa Ayatollah Imam Sayyid Ali Khamenei (ra) kwa ajili ya kushiriki katika ibada na shughuli za kumuenzi. Picha zinaonesha mazingira ya maombolezo na maandalizi yaliyoendelea kabla ya kuwasili kwa mwili huo Mtukufu... Waumini wakiwa katika hali ya huzuni na masikitiko, huku wakiwa wamebeba Picha za Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran Ayatollah Sayyid Ali Khamenei (Allah Amrehemu).

Your Comment